Thursday, September 18, 2014

UJUMBE MUHIMU KUTOKA KWA MKUU WA MSAFARA WA WASANII BUNGENI DODOMA, SIMON MWAKIFAMBA RAIS WA TAFF

TAARIFA KWA WASANII WOTE WA TANZANIA, NAOMBA IELEWEKE MCHAKATO WA HOJA ZA WASANII KUWEPO KWENYE RASIMU YA KATIBA SI KWA MASLAHI YA TAFF AU TDFAA NI KWA MASLAHI YA WASANII WOTE WA NCHI HII.KAMA UNAONA JAMBO HILI LINA MSLAHI UNGANA NASI,KAMA UTASHINDWA KWA KUTOKUWA NA UWEZO TUTAKUWAKILISHA NA KAMA HALIKUHUSU UBARIKIWE.SAFARI YA DODOMA IPO JUMAPILI 21 SEPTEMBA.SIMON J MWAKIFWAMBA KIONGOZI WA MSAFARA KWA SANAA ZOTE

Wednesday, September 17, 2014

NYAMAYAO AJA NA JOYCE

Msanii mkongwe aliyewahi kutamba sana katika kundi la Kaole Sanaa Group, amevunja ukimya anakuja na mzigo huu, hebu muunge mkono kwa kununua nakala halisi halafu uangalie uone ukweli wa msemo "Ng'ombe Hazeeki Maini"

ACTION & CUT VIEWERS CHOICE AWARDS 27TH SEPTEMBER 2014 SUNRISE BEACH KIGAMBONI





Popote duniani kinacholeta mvuto ni kile kinachoshindaniwa, hata mpira usingekuwa na mashindano, kusingekuwa na msisimko wala wapenzi wa soka...Kwa hatua hii nadhani kila mmoja atakuwa makini, ombi langu, chonde chonde tuzo hizi ziendelee. Maana nakumbuka kwa mara ya kwanza katika historia ya kiwanda cha filamu nchini kulikuwa na tuzo za Vinara mwaka 2008 baada ya hapo kimyaa!! Zikaja tuzo za Bora wa 2010 baada ya hapo kimyaa!! Zikaja tuzo za Steps mwaka 2013 baadae zii!! Sasa zamu ya Action & Cut Viewers Choice Awards, sijui baada ya hapo kaburi limeshachimbwa? Only God knows!! Ila Big up sana kwa waandaaji.www.facebook.com/Ali Yakuti