Wednesday, April 25, 2012

NYAKATI ZA KUKUMBUKWA

    Hapa nilikuwa namwelekeza kitu wakati wa upigaji picha ya                  Family Tears 2008

      “Hakuna kitu kizuri duniani kama kuifanya dunia hii kuwa darasa kwako, jifunze kwa kila mtu, hata kichaa aweza kuwa mwalimu kwako, kama hutajifunza chochote toka kwa kichaa basi hata kutoautisha tu mwenye akili kwa kumlinganisha na huyo kichaa ni darasa tosha…” 
      Nakumbuka maneno haya nilimwandikia Hayati Steven Charles Kusekwa Kanumba katika moja ya script chakwa zilizomkuza na ikawa ni dira katika maisha yake. Nitaikosa sana tabia yake hii ya kuwa msikilizaji kuliko mbishani, alipenda sana kujifunza na kudadisi mno kwa kitu ambacho hakukijua, hakuwa mjuvi kwa jambo asilojua, na akilijua basi hulizingatia, Tunapaswa kuiga tabia hii kama kweli tunataka kubakisha historia nyuma yetu.

1 comment:

  1. bro kiukweli nafurahia kuifanya dunia kuwa darasa kwangu, wewe umekuwa mwalimu kwangu pale ninapotamani kufanya kazi nzuri kama za kwako(uandishi bora wa script) na pia brother jb anazidi kuwa mwalimu kwangu pale ninapofikiria kuwa actor mkubwa kama yeye hvyo naifurahia dunia kuwa darasa huru kwangu nisilochangia hata shilingi kumi, Marehemu steven kanumba tutamkumbuka daima kwa kuipeleka sanaa yetu mbali na kututambulisha kimataifa kama isingekuwa mauti angeipeleka sanaa yetu hadi hollywood, ila kazi ya mungu haina makosa tumwombee alale salama katika makazi yake ya kudumu, naitwa Mussa mwakitinya

    ReplyDelete