Sunday, April 29, 2012

NYAKATI AMBAZO NI NADRA KUSAHAU


                               Mimi  na hayati Steven Kanumba baada ya kuchukua tuzo zetu mwaka 2010

         Kuna tatizo hili Tanzania, sijui niseme ni sugu au niliiteje? Hakuna chombo au taasisi maalumu inayohusika moja kwa moja na utoaji wa Tuzo za Filamu....Sijajua sababu hasa ni nini. Mwaka 1999, kulikuwa na Tuzo zilizojumuisha kada mbali mbali filamu ikiwa mojawapo, na ninakumbuka aliyeibuka kuwa msanii bora wa kiume alikuwa Richie Richie, wengine siwakumbuki pengine kwa sababu hawapo tena kwenye tasnia, tuzo hizo ziliandaliwa na M-net. Mwaka 2006 (Kama sikosei), kul,ikuwa na Tuzo za Risasi zilizoandaliwa na Gazeti lka Risasi, na msanii bora wa kiume alikuwa Dimoso, wakati msanii bora wa kike alikuwa Riyama. Mwaka 2008 kulikuwa na Vinara Awards ambapo Msanii bora wa kiume alikuwa Jacob Steven na Msanii bora wa Kike alikuwa (Simkumbuki jina) ila Irene Uwoya na Yusuf Mlela walipata tuzo ya up coming wakati Steven Kanumba akiambulkia tuzo ya heshima. Mwaka 2010 kulikuwa na tuzo za Filamu Central, ambapo Mimi nilishinda nafasi ya mwandishi bora wa Mwaka, Steven Kanumba alishinda Mugizaji bora wa Mwaka, Monalisa lishinda muigizaji bora wa kike wa mwaka, Vincent Kigosi alishinda tuzo ya muongozaji bora wa mwaka na mtayarishaji bora wa mwaka. Kukafuatia tuzo ambazo hazina utaratibu na hata zote ambazo nimekuwa nikizitaja huwa zinafanya mara moja halafu hazirudii tena, labda ZIFF kidogo naona wana utaratibu wa kuwa na tuzo kila mwaka, sijui sasa watu huandaa wakiwa wanatarajia kitu tofauti na uhalisia? Hebu tuchangieni

3 comments:

  1. unapoweka tuzo ambazo ni za kudumu zinaleta hamasa sana katika tasnia, mfano mzuri ni tuzo za kilimanjaro tanzania music award ni tuzo ambazo hutolewa na mdau mmoja ambaye ni bia ya kilimanjaro na zina hamasa kubwa katika tasnia ya filamu,hvyo imefika muda wa wadau wa tasnia ya filamu(cosota,makampuni na wizara husika) kuungana na kuanzisha tunzo ambazo zitadumu npaka milele kwani tukifanya hivyo tutakuwa tunaleta hamasa kubwa katika tasnia ya filamu, mimi yangu ni hayo tu!

    ReplyDelete
  2. kilimanjaro tanzania music award nikimaanisha tunzo zenye amasa katika tasnia ya mziki hvyo wadau wa filamu lazima waangalie hili swala kiundani

    ReplyDelete
  3. Hapo Kaka kwa mm nawezasema walikuwa waanfanya hivyo kwa manufaa yao na baaada ya kupata kile walichokitalajia wanachana na hilo swala mbona Kili ni za kila mwaka au hiz za Zanzibar Festival...! Zinakuwaa kila mwaka au zinaajirudia lakin nying hapo umezitajaa ni kweli sijazisikia tena tangu hapo, kwaahiyo nawezasema wanakuwa wanatafuta wanachokiaonaa kwao kinawanufaisha tu.

    ReplyDelete