Saturday, September 10, 2011

CHAMA CHA WAIGIZAJI WA FILAMU NA TAMTHILIYA MKOA WA KINONDONI KUZINDULIWA

CHAMA cha Waigizaji Mkoa wa Kinondoni kinazinduliwa rasmi siku ya jumatatu tarehe 12/ 9/ 2011 katika ukumbi wa Vijana Kinondoni, mkutano huu unawakutanisha wasanii wote wa eneo hili la Kinondoni kwa ajili ya usajili wa wasanii na kuutambulisha uongozi uliopo madarakani , siku hii pia itatumika katika kupanga mikakati katika kujiletea maendeleo. Katika mkutano huu mgeni wa heshima ni Naibu Waziri Wa Habari Vijana, Utamaduni Na Michezo Dk.Fenela Mukangara , pia siku hii utaendeshwa harambee kwa ajili ya kuchangia chama, kwa matumizi ya Chama hicho. Akiongea na FC Mwenyekiti wa Chama hiki Adam Melele (Swebe) amesisitiza wasanii kujitokeza kwa wingi kwani tayari mikakati ya kimaendeleo ndiyo hasa lengo la uanzishaji wa vyama ambavyo kwa sasa vipo katika michakato ya kuwaunganisha wasanii kwa kuwaongoza.
 "Tukiwa pamoja ni rahisi sana kujua matatizo yetu na njia sahihi katika kuyatatua, lakini bila umoja hakuna jambo litakalofanyika katika kuijenga sanaa hii, ambayo ni imani yetu kuwa endapo itatumiwa vema ni ukombozi kwa vijana” Swebe.
Mkutano utaanza saa nne kamili asubuhi katika ukumbi wa Vijana maeneo ya Kinondoni jirani na Mango Garden.

MTANZANIA ANAYETESA HOLLYWOOD HUYU HAPA.

                                                 Rachel Zawadi Ruttrell

Alizaliwa tarehe 19 januari mwaka 1971 Lushoto Tanga kwa baba Mmarekani kutoka Louisiana na mama Mtanzania. Familia yake ilihamia nchini Canada mwaka 1976, wakati yeye ana miaka mitano ambako ameendelea kuishi mpaka leo hii. Baba yake alikuwa mwanachama wa kikundi cha Toronto Mendelssohn choir, ambapo pia alimfundisha Rachel sauti ya soprano. Rachel pia alijifunza kucheza muziki aina ya ballet katika shule Russian Academy of Classical Ballet School, pia alijifunza kupiga piano katika shule ya Royal Conservatory of Music ya Toronto. Mafunzo ya muziki yalimvuta Rachel katika kuigiza, ambapo alianza kuigiza katika tamthiliya kama Miss Saigon, na baadae Goblin market na Once on this Island. Pia amepata sifa kubwa sana katika tamthiliya ya Stargate Atlantis...Kitu kikubwa kwake, anajivunia kuzaliwa Tanzania.

MZEE KIPARA TAABAN...MSAADA UNAHITAJIKA

                                      FUNDI SAID "MZEE KIPARA"
Unamfahamu msanii mkongwe Fundi Said, almaarufu kama Mzee Kipara, kama ni hivyo basi tunahitaji kumsaidia mzee wetu amekuwa akisumbuliwa miguu kwa muda mrefu sana kwa kifupi Mzee wetu anasumbuliwa na magonjwa mengi ila kwa sasa ni miguu ndio inayomsumbua sana kutoa ni moyo wa wala si utajiri mimi kwa upande wangu nitajitoa kwa hali na mali lakini pia bado tunaomba misaada kutoka kwa wasamalia wema kampuni Global Publisher iliweza kumpa cm ili haweza kutumia kwa njia ya M PESA ili iweze kumsaidia kwa urahisi zaidi namba ni 0753 923454 Asanteni sana.

MZIGO MPYA TOKA RJ COMPANY...UNPREDICTABLE



Kama lilivyo jina lake, mimi siwezi kupredict chochote kilichomo ndani ya filamu hii mpya kwa mwaka huu toka RJ Company, ingawa kama desturi ni kazi nyingine ya mkono wangu...Kitu pekee ninachoweza kukuahidi ndani ya mzigo huo ni kwamba, hautajutia pesa yako pale utakaponunua nakala yako halisi. Kazi imetulia tangu kisa chake, mtiririko wa matukio, ubora wa picha na hata midundo ya kusindikiza. Kazi kwako...Usiseme sijakuambia.

Naweza kusema watu hawa ndicho kioo changu

                                        Tyler Perry
       Mwandishi wa Filamu, michezo ya jukwaani na mwigizaji mahiri.



                                           Sidney Sheldon
                              Mwandishi mahiri wa Riwaya

Nakumbuka kuna mwalimu wangu mmoja aliwahi kuniambia kuwa, kama unataka kuwa mahiri katika jambo lolote lile, lazima uwe na mtu wa kumuiga (role model), na tangu nilipoambiwa hivyo, nimekuwa nikijaribu kujitafuta hasa mtindo ninaupenda sana huwa ninaupata wapi, nimejikuta nikigundua watu hawa wawili; mmoja akiwa mwandishi mahiri wa riwaya (novel); kitu ambacho nami pia nakifanya, mtu ambaye kabla hajaanza kuandika novel, alikuwa mwandishi wa filamu kwa miaka kumi na saba Hollywood na kupata tuzo kadhaa, mtu huyo ni Sidney Sheldon. Na mwingine akiwa ni mwandishi mahiri wa miswada ya filamu (script), pamoja na michezo ya jukwaani, ikiwa ni pamoja na kuigiza nafasi nyingi na kuzimudu vema. Mtu huyo ni Tyler Perry. watu hawa naweza kusema ni kioo changu katika sanaa.